Dhima ya futuhitandao katika kukabiliana na masuala ya afya ya akili miongoni mwa wakenya
Keywords:
Afya ya akili, dhima, futuhitandao, kukabiliana, masualaAbstract
Kiswahili
Fasihi kupitia utambuzi na tanzu zake tofauti tofauti, tangu jadi, imekuwa na majukumu mahususi ya kutekeleza katika jamii. Kama utanzu mojawapo wa fasihi simulizi, futuhi imetumika pakubwa katika vyombo vya habari kama vile televisheni na redioni kuwafurahisha na kuwachekesha watazamaji na wasikilizaji. Hata hivyo, katika siku za hivi karibuni, futuhi imechukua mkondo tofauti katika uwasilishaji wake. Hii ni kwa sababu ya njia mpya ya mawasiliano ya teknolojia ya kisasa ambayo imezua mitandao ya kijamii kama vile Facebook, TikTok, Twitter, Instagram na YouTube. Mbinu mpya za kiteknolojia sasa zipo kwa wingi kuliko wakati mwingine wowote. Licha ya mkurupuko wa mbinu hizi, tusisahau kwamba tangu jadi futuhi imekuwa muhimu katika jamii mbalimbali. Lakini sasa futuhi imekuwa karibu zaidi kwa sababu ya teknolojia ya kisasa. Vile vile, suala la afya ya akili limekuwa nyeti miongoni mwa Wakenya. Hivyo basi, kukawa na haja ya kuchunguza zaidi kuhusu futuhi katika mitandao hii ya kijamii na afya ya akili miongoni mwa Wakenya. Mada hii vile vile ilichaguliwa kwa sababu tafiti ambazo zilihusu futuhi, ziliegemea futuhi katika vitabu vya riwaya na tamthilia na hazikujikita katika suala la afya ya akili. Hivyo basi, makala haya yalinuia kujaza pengo hili kwa kutafitia futuhitandao na afya ya akili miongoni mwa Wakenya, na hasa kwa kuzingatia futuhi zinazopatikana kwenye mitandao ya kijamii hususan Facebook, Twitter na YouTube. Makala haya yalitumia nadharia ya Burudiko ya Sigmund Freud. Utafiti huu ulitumia muundo wa kiethnografia, mkabala wa kithamano. Data kuhusu futuhitandao ilikusanywa kwa mbinu ya Uchanganuzi wa Yaliyomo. Uteuzi wa sampuli ulikuwa wa kimakusudi na kinasibu. Umuhimu wa makala haya ni kuwa, matokeo yake yatasaidia katika ufundishaji wa futuhi. Inapendekezwa kuwa tafiti zaidi zifanywe kuhusu suala la afya ya akili kwa kurejelea vipera vingine vya fasihi simulizi.
English
Art in its various realization and genres from time immemorial, has had distinct social roles to play. Joke performance, as one of the oral literature genres, has been used at large through media such as television and radio to entertain viewers and listeners. But in the recent times it has taken a different way of presentation. This is because of the numerous ways of communication such as Facebook, Twitter, TikTok, Instagram and YouTube, as a result of the new technology. Nowadays we have many ways of communication than ever before, because of the new technology. Besides this new evolution of ways of communication, let us not forget that comedy has been of great importance to our society and it has been used to tackle many emerging issues that affect the society in Kenya. So there was a greater need, to do a research concerning online comedy and mental health among Kenyans, this is because mental health has become such a big issue in our country. The purpose of this study was to show the role of online comedy and how it can be used to tackle issues related to mental health among Kenyans. This research topic was picked because those who researched on comedy dwelled on literature books, that is, novels and plays. This research therefore aimed at filling the gap by studying online comedy and mental health among Kenyans. The study was guided by humour theory of Sigmund Freud. This research adopted descriptive case study design. The study was carried out through social media platforms specifically Facebook, Twitter and YouTube. Purposive and random sampling techniques were used. This research used content analysis guide, as its method of data collection. This research showed that there is relationship between online comedy and mental health among Kenyans, from the data that was collected, and that, online comedy as any other genre has various roles to play. More studies can be done on online comedy in relation with other oral literature genres.
Keywords: Issues, mental health, online comedy, role, tackle
Downloads
Published
How to Cite
Issue
Section
Copyright (c) 2025 Emilly Magambo, Fred Simiyu, Felix Orina

This work is licensed under a Creative Commons Attribution-NonCommercial-ShareAlike 4.0 International License.