Uhalisia katika mashairi ya Kezilahabi (Dhifa)

https://doi.org/10.51317/eajk.v4i1.183

Authors

Keywords:

tamathali za usemi, tashihisi, Uhalisia

Abstract

SWAHILI

Fasihi ni kioo cha maisha. Humulika jinsi jamii ilivyo kwa kuangazia masuala mbalimbali yanayoikumba. Waandishi wa kazi za fasihi huchota maudhui yao kutokana na matukio mbalimbali yanayoikumba jamii, nia yao ikiwa ni kuielimisha, kuiadilisha na kubeza maovu yanayotendeka. Makala hii inaangazia uhalisia katika mashairi ya Diwani ya Dhifa iliyoandikwa na Euphrase Kezilahabi (2008). Kupitia kwa mashairi yake, Kezilahabi ameichora hali halisi iliyopo katika mataifa mengi ya Afrika kwa kumulika matatizo mbalimbali yanayoyakumba. Anaupitisha ujumbe wake kwa kutoa taswira nzito zinazoundwa kutokana na matumizi ya tamathali mbalimbali za usemi ambazo zinaacha athari kubwa kwa wasomaji na kuwachochea kupata ari ya kupigania haki za wanyoge. Utafiti huu unaongozwa na nadharia ya uhalisia, ambayo kulingana na Wamitila 2002, iliwekewa msingi na mwanafalsafa Hegel katika kitabu chake kinachojulikana kama Aesthetik. Utafiti unawawezesha wanajamii hasa kutoka mataifa ya Kiafrika kuyabaini matatizo mbalimbali wanayokumbana nayo na jinsi ya kujinasua kutokana na minyororo ya umaskini.

ENGLISH

Literature is the mirror of society. It reflects the various issues that propel or ail society. Literary scholars derive various thematic concerns from the happenings in society with the view to educating, edifying and shunning unbecoming behavior in our society. This study focuses on realism in Euphrase Kezilahabi’s book, Dhifa. Kezilahabi, through his poems, depicts the economic, political and social realities affecting African countries. He employs striking imageries and literary stylistic features, which have positive effects on his readers, impelling them to advocate for their rights. This study is guided by realism theory, which according to Wamitila (2002), relies heavily on Hegel’s publication, The Aesthetics. The study will highlight on problems facing Africans as well their solutions.

Key terms: imageries, realism, stylistic features                                          

Downloads

Download data is not yet available.

Published

2022-08-15

How to Cite

Maithya, J. K. (2022). Uhalisia katika mashairi ya Kezilahabi (Dhifa). Eastern Africa Journal of Kiswahili (EAJK), 1(1), 43–49. https://doi.org/10.51317/eajk.v4i1.183

Issue

Section

Articles