Kuwezeshwa kwa uchumi kupitia lugha ya kiswahili

https://doi.org/10.51317/eajk.v4i1.40

Authors

Keywords:

Lugha, utamaduni, mawasiliano, maendeleo na uchumi

Abstract

SWAHILI

Makala haya yanalenga kuangazia juhudi za nchi za Afrika mashariki na bara la Afrika kutumia Kiswahili kama nyenzo ya mawasiliono miongoni mwao ili kurahisisha mawasiliano na biashara kati ya wananchi wa mataifa haya. Makala haya yametumia data za kimsingi za tafiti za awali katika kufikia hitimisho lake. Lugha nyingine zinazozungumzwa Afrika masharika kando na lugha-mame za wazaliwa wa Afrika mashariki ni, Kiingereza, Kifaransa na Kijerumani. Lugha hizi zilizokuja na mkoloni pia zimepata nafasi kubwa katika jamii ya Afrika kwa ujumla. Siku za hivi karibuni kumeshuhudiwa ongezeko la matumizi ya lugha ya Kichina na mafunzo kutolewa kwa waafrika kwa lugha hii. Hata hivyo, lugha hizi zinaendelezwa kwa mtazamo na imani za waafrika wenyewe. Waafrika wengi wanaamini kuwa, maendeleo na kungeuka kunatokana na lugha hizi za kikoloni. Mitazamo hii ni tata na imelifanya bara la Afrika kuyumba kimaendeleo. Baadhi ya nchi za Afrika zinatumia lugha za kikoloni kama lugha zao rasmi. Hili linalazimisha yeyote anayezuru nchi hizi ajifunze lugha yao ili kuwepo mawasiliano. Hatua zinazochukulia na nchi za Afrika kutafuta lugha ya kutumika katika nchi zote Afrika ni juhudi za kupewa nguvu na kuungwa mkono na kila nchi ya Afrika. maendeleo hutegemea mawasiliano bora na ambayo hufanikishwa na lugha. Kiswahili kuwa lugha yenye asili ya Kiafrika na juhudi hizi za maenezi kutoka kwa nchi za kiafrika basi itakuwa kiunganishi bora cha nchi hizi.

Downloads

Download data is not yet available.

Published

2022-07-06

How to Cite

Sawe, A. J. (2022). Kuwezeshwa kwa uchumi kupitia lugha ya kiswahili. Eastern Africa Journal of Kiswahili (EAJK), 1(1), 1–5. https://doi.org/10.51317/eajk.v4i1.40

Issue

Section

Articles

Similar Articles

1 2 > >> 

You may also start an advanced similarity search for this article.