Uchanganuzi wa vipashio vya mamlaka katika midahalo ya siasa za uchaguzi wa 2022 nchini Kenya kwenye jukwaa la kidijitali la youtube

https://doi.org/10.51317/eajk.v3i1.562

Authors

Keywords:

kampeni, mamlaka, midahalo, vipashio, wanasiasa

Abstract

SWAHILI

Makala hii inalenga kutambua mchango wa lugha kama chombo kinachodhihirisha mamlaka katika jamii kwa kuchanganua baadhi ya vipashio vilivyodhihirisha mamlaka katika midahalo ya wakati wa uchaguzi wa 2022 nchini Kenya kama inavyojitokeza katika jukwaa la kidijitali la Youtube. Wanasiasa wana hulka ya kutumia lugha yenye kupendeza kwa wananchi nyakati za kampeni kwa njia ya kipekee ili kubadilisha mawazo yao. Katika harakati hizi, wanasiasa huvuta mamlaka upande wao kwa njia isiyo wazi. Hali hii huwafanya wasikilizaji wengi kukosa kuelewa habari iliyotolewa kwa kutoelewa vipashio vilivyotumiwa katika hotuba hizo, hivyo kufanya maamuzi mabaya kisiasa. Utafiti huu ulizingatia muundo wa kiuchanganuzi kwa kutathmini data za kiuthamano zitakazoelezwa kinathari. Eneo la utafiti ni la kitaaluma. Kundi lengwa la utafiti ni midahalo ya wanasiasa wakati wa kampeni za uchaguzi wa mwaka wa 2022 nchini Kenya. Usampulishaji wa kimaksudi ulitumika huku data zikikusanywa kutoka kwenye mtandao wa youtube kwa mbinu ya uchanganuzi wa yaliyomo na kuwasilishwa kimaelezo. Makala hii ilibainisha kuwa japo siasa huwasisimua wananchi na midahalo yake kuwavutia kwa wingi, wengi wao hukosa kuelewa kabisa wayasemayo wanasiasa hawa huku wengine wakipata ufasiri potovu. Data zilizokusanywa zitasaidia katika kudhihirisha sababu za wananchi kutoelewa habari fiche ambazo huwasilishwa na wanasiasa katika midahalo yao, ambacho ndicho chanzo cha wananchi kutoelewa habari hizo na hivyo kufanya maamuzi mabaya kwa kuwachagua viongozi wasiofaa.

ENGLISH

Politicians have the tendency to use language that appeals to the people during campaigns in a unique way to change the minds of the people, so that they can accompany their wishes to control them behaviorally and ideologically while aiming to increase their popularity and convince the people to support them. In such, politicians pull power to their side in an unclear way, a situation that causes many listeners to fail to understand the information given by not understanding the terms used in those speeches, thus making bad political decisions. Power is evident where there are conflicting opinions between politicians. This article therefore aims to identify the contribution of language as a tool that demonstrates power in society by analyzing some of the tenets that demonstrated power and authority in the political discourses during the 2022 election in Kenya as it appears in the YouTube digital platform. This study will focus on the analytical design by evaluating the relational data that will be described in prose. The study is based on the academic research area. The target group of the research are the debates of politicians during the 2022 election campaigns in Kenya. Purposive sampling will be used while the data will be collected from the You-tube network using content analysis method and presented descriptively. The data that will be collected will help in revealing the reasons why citizens do not understand hidden information that is presented by politicians in their debates, which is the source of citizens not understanding the information and therefore making bad decisions by choosing the wrong leaders.  This article will be involved in solving the problem of citizens not understanding the specific information of politicians in their face-to-face debates.

Downloads

Download data is not yet available.

Published

2024-09-20

How to Cite

Aboge, A. N., Miruka, F., & Jagero, J. A. (2024). Uchanganuzi wa vipashio vya mamlaka katika midahalo ya siasa za uchaguzi wa 2022 nchini Kenya kwenye jukwaa la kidijitali la youtube. Eastern Africa Journal of Kiswahili (EAJK), 3(1), 30–41. https://doi.org/10.51317/eajk.v3i1.562

Issue

Section

Articles