Mageuzi ya Kimofolojia ya Msamiati wa Mame-Bantu kwenda Lugha za Kibantu: Mifano kutoka Kinyakyusa

https://doi.org/10.51317/eajk.v5i1.993

Authors

Keywords:

Mageuzi ya kimofolojia, Mame-Bantu, Kinyakyusa

Abstract

Makala hii inahusu mageuzi ya kimofolojia kutoka Mame-Bantu (MB) kwenda Kinyakyusa. Lengo la utafiti huu lilikuwa kuchunguza mabadiliko ya kimofolojia ya maumbo ya vitenzi na nomino kutoka MB kwenda lugha ya Kibantu. Utafiti huu ni wa kitaamuli na uliongozwa na Nadharia ya Mofolojia Asilia ya Wolfgung U Dressler (1987). Data za utafiti zilikusanywa kwa njia ya uchambuzi wa matini pamoja na usaili wa wazungumzaji asilia wa Kinyakyusa. Jumla ya maumbo ya msamiati 35 ya MB yalichambuliwa kutoka kwenye matini ya Bostoen na Bastin (2016), kisha kufasiriwa kwa Kinyakyusa. Aidha, usaili uliofanyika kwa wazungumzaji asilia sita (06) wa Kinyakyusa ulilenga kupata tafsiri ya maumbo ya vitenzi na nomino zilizochunguzwa. Sampuli ya utafiti iliteuliwa kwa kutumia usampulishaji lengwa wa kipekee na kwa kuzingatia vigezo vya umri, jinsi na umahiri wa lugha. Matokeo ya utafiti yalionesha kuwapo kwa mageuzi ya kimofolojia ya msamiati wa MB kwenda Kinyakyusa. Mageuzi haya yanachagizwa na mabadiliko ya vitamkwa kama vile vipasuo kuwa vipasuo kwamizi kupitia uyeyushaji wa irabu. Pia, kipasuo kuwa likwidi au sauti za likwidi kutokana na uimarishaji au udhoofishaji wa konsonanti. Vilevile, uchunguzi ulibaini kuwapo kwa mageuzi si-kamilifu ambayo huhifadhi umbo asilia la mzizi wa neno la MB katika lugha ya Kinyakyusa. Pia kulibainika kuwapo kwa mageuzi kamilifu ya kimofolojia ambayo hayahifadhi umbo asilia la msamiati wa MB katika lugha za Kibantu. Kwa kuwa utafiti huu ulijikita katika umbo la msamiati pekee, tafiti zingine zijazo zinaweza kuchunguza kuhusu mageuzi na/au uhifadhi wa maana kupitia toni na miundo ya tungo kutoka Mame-Bantu kwenda lugha nyingine za Kibantu, kikiwamo Kiswahili.

Downloads

Download data is not yet available.

Published

2026-06-12

How to Cite

Deogratius, E. (2026). Mageuzi ya Kimofolojia ya Msamiati wa Mame-Bantu kwenda Lugha za Kibantu: Mifano kutoka Kinyakyusa. Eastern Africa Journal of Kiswahili (EAJK), 5(1), 65–78. https://doi.org/10.51317/eajk.v5i1.993

Issue

Section

Articles